PATA POWER BANK ZENYE UBORA WA HALI YA JUU KWA BEI NAFUU ZAIDI

PATA POWER BANK ZENYE UBORA WA HALI YA JUU KWA BEI NAFUU ZAIDI

Sunday, December 7, 2014

Taarifa nzuri leo kwenye usafiri kwenda Kigoma,Mwanza...


Hitachi-Standard-Class-AYes, good news nyingine Tanzania.
Katika ile ahadi ya jitihada za Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi kuboresha miundombinu za usafirishaji nchini, leo kuna taarifa nyingine nzuri juu ya kile ambacho Wizara hiyo imekifanya kwenye sekta ya usafirishaji ambapo yamewasili mabehewa 50 mengine tayari kwa kuanza kutoa huduma.
… Ile ndoto tuliyokuwa tunaitegemea kwa muda mrefu sasa imeanza kutimia tuna vichwa vya treni 13 ambavyoo tunavitegemea muda wowote ambavyo vitaongezwa nguvu na vile ambavyo vitaongeza nguvu na vile vichwa ambavyo tunavitengeneza Morogoro, tulianza na vinane tumemaliza tunaingiza vingine vinane kwa hiyo nguvu ya TRL mnaiona inaanza kuja polepole…” Dk. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Uchukuzi.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TRL, Kiparo Kisamfu amesema; “Haya mabehewa ni kwa ajili ya safari za kwenda Mikoani hususan Kigoma na Mwanza lakini nia yetu ni kuanzisha treni maalum ambayo unaweza kuiita deluxe train ambayo tunatarajia itasimama kwenye vituo vikubwa tu, haitokuwa kama zile treni mbili zinazotembea sasa hivi… Na kwenye mabehewa haya kila mtu atakaa kwenye kiti chake hakuna mtu atakayesimama na yatachukua muda mfupi Zaidi kufika Kigoma na Mwanza kama ilivyo sasa hivi…

No comments:

Post a Comment