PATA POWER BANK ZENYE UBORA WA HALI YA JUU KWA BEI NAFUU ZAIDI

PATA POWER BANK ZENYE UBORA WA HALI YA JUU KWA BEI NAFUU ZAIDI

Monday, September 8, 2014

Mourinho asema Chelsea haitawaiga Manchester United.


London, England. Kocha Jose Mourinho amesema kamwe hawezi kufanya mambo yake katika usajili kwa kuwaiga mahasimu wao, Manchester United, ambao wanatumia fedha nyingi kwa sasa.
Chelsea ilianza usajili wao mkubwa kwa kuwanasa nyota wa Hispania, Diego Costa na Cesc Fabregas mapema kabla ya Kombe la Dunia.
Lakini bosi huyo wa Chelsea alisema hata katika usajili wa Januari atarudia alichofanya awali kwa kuwa miamba hiyo haiko tayari kwa sasa kutoa fedha zaidi katika usajili.
Mourinho alihusisha sheria ya uungwana katika matumizi kuwa inaweza kuifunga Chelsea kwa kuwa timu inayoweza kutumia fedha zaidi, huku akisisitiza kuwa hawawezi kufikia rekodi ya Pauni 60 milioni iliyowekwa na United walipomsajili Angel Di Maria. Usajili wa Di Maria ulivunja rekodi iliyowekwa na Chelsea 2011 ilipomsajili Fernando Torres kwa Pauni 50 milioni.
“Tunatengeneza fedha ili tuweze kuzitumia. Katika kila dirisha la usajili Chelsea inapoteza wachezaji, inauza wachezaji,” Mourinho aliliambia Eurosport.
Matumizi ya Chelsea yako mbali na ya Manchester United, ambao wametumia fedha nyingi kusajili wachezaji kama Di Maria na Luke Shaw msimu huu, wakati Blues wakitumia Pauni 30 milioni za mkataba wa kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas, ambapo inazidiwa na Pauni 75 milioni wanazopata United katika udhamini.
Lakini Mourinho hana tatizo katika mpango wake wa kusitisha matumizi ya fedha kutokana na kulizoea hilo alipokuwa na klabu ya Porto.
“Chelsea kwa sasa si watumiaji wa fedha nyingi. Kwa sasa tunatengeneza fedha nyingi katika dirisha la usajili kuliko tunazotumia kununua wachezaji.
“Hivyo kwa sasa Real Madrid, Barcelona, Bayern, Manchester (United) ndizo zinazotumia fedha nyingi, nadhani wana nafasi katika hilo,” alisema.

No comments:

Post a Comment