PATA POWER BANK ZENYE UBORA WA HALI YA JUU KWA BEI NAFUU ZAIDI

PATA POWER BANK ZENYE UBORA WA HALI YA JUU KWA BEI NAFUU ZAIDI

Sunday, November 4, 2012

UJENZI WA BARABARA WATOA AJIRA 650,000



WAZIRI wa Ujenzi, Dk John Magufuli amesema miradi mikubwa ya ujenzi wa barabara inayoendelea nchini na yenye urefu wa kilometa 11, 154, imetoa ajira kwa watu 650,000.

Aidha, Dk Magufuli amesema ujenzi huo mkubwa wa barabara, ndiyo tafsiri sahihi ya kaulimbiu maarufu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Maisha Bora kwa Kila Mtanzania.
Dk Magufuli alisema tofauti na mawazo ya baadhi ya watu, miradi hiyo mikubwa ya ujenzi wa barabara inagharimiwa kwa asilimia 60 na Serikali ya Tanzania.

Waziri Magufuli aliuambia mkutano wa hadhara uliofanyika juzi katika kijiji cha Nanja mkoani Arusha wakati wa uzinduzi wa mradi wa ukarabati mkubwa wa Barabara ya Minjigu-Arusha kuwa miradi ya ujenzi pekee yake imezaa ajira 650,000. Wananchi pengine watu hawajui, lakini nataka kuwaelezeni kuwa katika Wizara moja tu ya Ujenzi kiasi cha ajira 650, 000 zimepatikana kutokana na miradi mikubwa ya barabara inayoendelea kujengwa nchini ya kiasi cha kilomita 11,154,” alisema Dk Magufuli Kuhusu maisha bora, alisema “Watu wanakejeli kaulimbiu ya maisha bora, lakini sisi katika CCM tunaposema maisha bora hakuna maana ya Serikali kugawa fedha kwa wananchi, bali ni Serikali kuwezesha wananchi. Maisha bora ni barabara, maisha bora ni usafiri wa wananchi wa uhakika kwenye barabara za lami, maisha bora ni usafirishaji mizigo usiokuwa na matatizo. Haya ndiyo maisha bora”

Aliwaambia wananchi kuwa uwezo wa Serikali kuhudumia barabara na kujenga barabara hasa za vijijini umeongezeka kwa kiasi kikubwa katika miaka saba iliyopita

Wakati uongozi wa sasa unaingia madarakani mwaka 2005, Mfuko wa Barabara ulikuwa na kiasi cha shilingi bilioni 54, lakini mwaka huu, kiasi hicho kwenye Mfuko huo kimefikia shilingi bilioni 430. Haya ni mafanikio makubwa sana na yanaongeza uwezo wa Serikali kuhudumia na kujenga barabara,” alieleza. Wakati huo huo, Rais Jakaya Kikwete janai alizindua miradi mbalimbali ya maendeleo katika mikoa ya Arusha na Manyara, ikiwa ni sehemu ya ziara zake za kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Singida.

No comments:

Post a Comment