PATA POWER BANK ZENYE UBORA WA HALI YA JUU KWA BEI NAFUU ZAIDI

PATA POWER BANK ZENYE UBORA WA HALI YA JUU KWA BEI NAFUU ZAIDI

Tuesday, November 6, 2012

BANDARI YAONGOZA KWA RUSHWA YA UNUNUZI VIFAA

MAMLAKA ya Bandari Tanzania (TPA), imetajwa kuongoza kwaviashiria vya rushwa katika ununuzi wa bidhaa na huduma unaosimamiwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA).



Mkurugenzi Mtendaji wa PPRA, Ramadhani Mlinga alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ukaguzi wa ununuzi katika taasisi za umma uliofanyika hadi Juni 30.

Mlinga alisema walipotumia kanuni za kupima rushwa katika ununuzi, TPA ilibainika kuongoza miongoni mwa taasisi za umma zilizokutwa na viwango vya juu vya uwezekano wa kuwapo rushwa kwa zaidi ya asilimia 20 ya shughuli za ununuzi.

Mbali na TPA iliyokuwa na asilimia 44 ya viashiria vya rushwa, ilifuatiwa kwa karibu na Wizara ya Mambo ya Ndani katika mradi wa ujenzi wa makao makuu ya kikosi cha Zimamoto iliyokuwa na asilimia 41 ya viashiria vya rushwa.



Taasisi ya tatu kwa kuwa na viashiria vingi vya rushwa kwa mujibu wa PPRA, ni Wizara ya Maji na Umwagiliaji katika mradi wa maji Chalinze iliyokuwa na asilimia 40.

Nyingine ni Halmashauri ya Wilaya ya Kyela (28%), Halmashauri ya Wilaya ya Makete (27%), Halmashauri ya Jiji la Mbeya (28%), Halmashauri ya Wilaya ya Tabora (20%), Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe (28%), Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (27%) na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga (23%) Kuhusu ukaguzi wa miradi kwa thamani ya fedha, Mlinga alisema kati ya miradi 137 iliyokaguliwa, ni miradi 63 tu ndiyo ilitekelezwa kwa thamani ya fedha na kwa mujibu wa mkataba.

Alisema asilimia 49 ya miradi hiyo, utekelezaji wake ulikuwa wa wastani ambapo miradi saba sawa na asilimia 5, utekelezaji wake haukuridhisha kabisa.

Sh bilioni 2 zayeyuka.



Kuhusu malipo yanayotia shaka, Mlinga alisema ukaguzi huo umebaini kuwa kuna taasisi kumi zilizofanya malipo yenye shaka ya Sh bilioni 2.1 kwa makandarasi.

Alitaja taasisi hizo kuwa ni Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga, Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero, Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya na Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro.

Nyingine ni Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Halmashauri ya Mji wa Kibaha, Wakala wa Vizazi na Vifo (RITA), Mfuko wa Akiba kwa Wafanyakazi wa Serikalini (GEPF) na Halmashauri ya Wilaya ya Chato.

SUMA JKT yafungiwa.

Mlinga alisema PPRA pia imefungia kampuni nne kushiriki zabuni zinazotangazwa na taasisi za umma kwa mwaka mzima baada ya kushindwa kutekeleza masharti ya mikataba yao katika zabuni walizowahi kupewa na kusababisha mikataba yao kuvunjwa.

Kampuni hizo ni pamoja na Shirika la Uzalishaji JKT (SUMA JKT) ya Dar es Salaam, Vector International ya Mwanza, Shy Builders Limited ya Shinyanga na Earthline Construction Limited ya Bukoba.

No comments:

Post a Comment