PATA POWER BANK ZENYE UBORA WA HALI YA JUU KWA BEI NAFUU ZAIDI

PATA POWER BANK ZENYE UBORA WA HALI YA JUU KWA BEI NAFUU ZAIDI

Sunday, June 30, 2013

Brazil yamshushia Hispania kipigo cha mbwa mwizi





Timu ya Taifa ya Brazili imeendeleza rekodi yake yakutofungwa katika michuano ya Kombe la mabara iliyokuwa ikifanyika nchini humo, hasa baada yakuipiga bila huruma timu ya Hispania ambayo ndiyo timu iliyotwaa ubingwa wa ulaya na dunia.
Brazili walionekana kuutawala mpira kwa kiasi kikubwa, na kunako dakika ya pili ya mchezo huo brazili ilipata bao la kuongoza kupitia kwa mshambuliaji wake Fred. Karamu hiyo ya magoli iliendelea kunako dakika ya 44 kupitia kwa mshambuliaji hatari Neymar aliyefunga goli zuri kwa mguu wake wa kushoto.
Kunako dakika ya 46 mshambuliaji Fred aiipatia brazil bao la tatu.
Mpaka kipyenga cha mwisho kinapulizwa, Brazili wakawa wameibuka na ushindi huo mnono ambao umeharibu rekodi ya Hispania ya kutofungwa mechi 29.
Brazili imefanikiwa. Kutetea kombe hilo ililolichukua nchini Brazili ikiifunga timu ya USA katika mchezo wa fainali.

No comments:

Post a Comment